Jarida la Al-Waie: Vichwa Vikuu vya Habari vya Toleo (468)
- Imepeperushwa katika Jarida la Al-Waie
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
Abu Ubaidah Aamir bin Abdullah bin Al-Jarrah Al-Fihri Al-Qurashi (40 Kabla ya Hijra/584 M hadi 18 Baada ya Hijrah/639 M) alikuwa Swahaba (ra) wa Mtume (saw), kamanda wa Kiislamu, na mmoja wa Maswahaba kumi (ra) waliopewa bishara njema ya Pepo. Alikuwa miongoni mwa watu wa kwanza kusilimu.
Maisha haya ya dunia ni kama dimbwi la hasara, ambalo ni wale tu wanaojua kukamata fursa ndio wataokolewa. Kwa sababu hii, Siku ya Kiyama inaitwa “Siku ya Majuto,” kwa sababu watu wengi wamezama katika hasara ya kidunia, na wameshindwa kutumia fursa za thamani walizopewa katika maisha yao. Walipoteza kwa urahisi nyakati za dhahabu alizozitoa Mwenyezi Mungu (swt) kwa ajili ya mwamko na izza ya Umma.