Gazeti la Al-Raya: Vichwa Vikuu vya Toleo 535
- Imepeperushwa katika Al-Rayah
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Dola ya Kiislamu imeegemezwa kwenye Aqidah (itikadi) ya Kiislamu, na hili linahitaji kwamba katiba yake na sheria zake zote zichukuliwe kutoka katika Kitabu cha Mwenyezi Mungu na Sunnah za Mtume Wake (saw).
Kwa kuzingatia mauaji ya kikatili (mauaji ya halaiki) ambayo yanayofanywa na umbile nyakuzi la Kiyahudi dhidi ya Waislamu wasio na ulinzi katika Ukanda wa Gaza na Ukingo wa Magharibi katika Ardhi Iliyobarikiwa (Palestina), na kwa kuzingatia matakwa ya adui wa Mwenyezi Mungu, Trump, kuwahamisha Waislamu wasio na ulinzi kutoka Ukanda wa Gaza, Hizb ut Tahrir/Wilayah Uturuki inaandaa amali za halaiki kote nchini Uturuki chini ya kichwa: “Ni Nani atamzuia Trump?!”
“Mapema leo, Rais Trump wa Marekani alithibitisha mpango wake wa Marekani kuchukua udhibiti wa Gaza na kuwafukuza Wapalestina, akisema kwamba amejitolea kuinunua na kuimiliki Gaza. Kauli hii ilitolewa na Trump mnamo Jumapili jioni ndani ya ndege ya Air Force One alipokuwa akielekea New Orleans kuhudhuria Super Bowl." (BBC, 10/2/2025) Baadaye, wakati wa mkutano wake na Mfalme wa Jordan, alisema: "Wapalestina wataishi kwa usalama mahali pengine, nje ya Gaza, na ninaelewa kwamba tuna uwezo wa kufikia suluhisho,"
Trump na Mfuasi wako Netanyahu: Macho Yako Yamepofushwa, umesahau hatima ya watangulizi wako miongoni mwa Warumi na Wafursi, pamoja na washirika wako duni, Mayahudi!
Ripoti ya jibu la swali lililotolewa na Amiri wa Hizb ut Tahrir, Mwanachuoni Mkubwa, Ata bin Khalil Abu Al-Rashtah, Mwenyezi Mungu amhifadhi, kuhusu Kuongezeka kwa Uhasama nchini Sudan.
Ramadhan ni mwezi ambao ndani yake Umma wa Kiislamu ulishinda maadui wengi wenye nguvu. Hebu Waislamu na waregeshe hukmu kwa Kitabu cha Mwenyezi Mungu ﷻ katika mwezi wa Ramadhan, na warudishe ushindi dhidi ya maadui, kwa kumtegemea Mwenyezi Mungu ﷻ.
Hii ni video iliyoelekezwa kwa wanasiasa wa Sweden kuhusu tishio linaloongezeka kwa Waislamu baada ya maneno ya chuki. Inakuja kama jibu kwa ufyatuaji risasi wa hivi punde wa shule huko Örebro.
Al Arabiya Net ilichapisha kwenye tovuti yake mnamo tarehe 4/2/2025: "Jeshi na vikosi vyake vya usaidizi viliingia katika maeneo ya kusini-mashariki ya Jimbo la Khartoum wakati wa saa zilizopita, wakitokea Jimbo la Al-Jazeera.." na tovuti ya Youm7 ilichapishwa mnamo tarehe 2/2/2025: "Mwandishi wa Kituo cha Habari cha Cairo aliripoti katika habari mpya zinazochipuka kwamba jeshi la Sudan linachukua idadi kadhaa ya vijiji mashariki mwa mto Nile katika Jimbo la Khartoum." Kabla ya hapo, mnamo tarehe 11/ 1/2025, Vikosi vya Msaada wa Haraka vilishindwa na jeshi la Sudan katika mhimili wa Jimbo la Al-Jazeera na mji mkuu wake, Wad Madani, “na kamanda wa Vikosi vya Msaada wa Haraka, Hemeti, alikiri katika kanda ya sauti iliyohusishwa naye kwamba vikosi vyake vilishindwa katika Jimbo la Al-Jazeera...” (Al-Jazeera 1/13/2025).