Jumapili, 23 Safar 1447 | 2025/08/17
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Tarehe 5 Agosti 2024 ni Siku ya Uasi wa Watu dhidi ya Dhalimu na Utawala wa Kidhalimu, ambao ungali Unaendelea; kinachojulikana kama 'Tangazo la Julai' ni Hati ya Usaliti wa Vyama vya Kisiasa vinavyounga mkono Marekani ili kuangamiza Uasi wa Watu

Wananchi wakiwa wamekata tamaa sana, wamepita mwaka mmoja tangu kuanguka kwa Hasina katika uasi mkubwa dhidi ya dhalimu Hasina na utawala dhalimu mnamo Agosti 5, 2025. Kwa sababu baada ya kuanguka kwa dhalimu Hasina, vibaraka wa Marekani na vyama vya kisiasa vyenye uchu wa madaraka vimechukua mshiko wa kubainisha hatima ya watu na kuweka vikwazo katika kutekeleza matumaini na matarajio ya watu na wameendelea na majaribio yao maovu na kuteka nyara uasi huo. Kinachojulikana kama 'Tangazo la Julai' ni hatua isiyo na aibu ya jaribio hili ovu. Watu wamekataa utumwa wa Marekani na sarakasi za kisiasa kwa chuki. Yaliyo mbali na kuakisi matarajio ya watu, Tangazo hili la Julai halitambui hata matukio kama vile njama ya India huko Pilkhana na mauaji ya halaiki ya watu wanaopenda Uislamu huko Shapla Chattar.

Soma zaidi...

Ni Lazima ikumbukwe kwamba Marekani ni Nchi ya Kikoloni; Kujisalimisha kwa Sera zake za Ushuru Kutahatarisha Ubwana wa Taifa!

Marekani, mchuuzi wa kimataifa wa ubepari, imeibua 'dhoruba ya ushuru' duniani kote, ikipuuza kanuni za uchumi wa soko huria – moja ya falsafa kuu za ubepari – na sheria na kanuni za kile kinachojulikana kama Shirika la Biashara Duniani (WTO) ililounda. Hii, kwa mara nyingine, inathibitisha kwamba mfumo wa kibepari hauna utu na wa kinyonyaji. Serikali ya mpito ya Bangladesh imetabanni sera ya utiifu katika kukabiliana na hatua za ushuru za Marekani. Tayari wamefanya uamuzi wa kujitoa mhanga kununua ndege 25 za gharama kubwa aina ya Boeing, pamoja na kuagiza pamba na LNG kutoka Marekani, ingawa nchi nyingi zinaghairi oda zao kutokana na utendakazi duni wa Boeing. Na wanafanya mikutano ya moja kwa moja na Marekani, wakiweka umma katika giza kupitia 'makubaliano fiche ya kihistoria' (NDA).

Soma zaidi...

Mkasa wa Milestone: Watoto Wasio na Hatia na Rubani wetu Jasiri Tauqir, walikuwa Waathiriwa wa Ukatili wa Kukosekana kwa Dola yenye kujali inayowachunga Watu

Jumatatu iliyopita (21 Julai, 2025) alasiri, ndege ya kivita ya Jeshi la Anga la Bangladesh F-7 BGI iligonga jengo katika sehemu ya chini ya Shule ya Milestone na Chuo katika eneo la Uttara katika Mji Mkuu kutokana na hitilafu ya kiufundi. Hii ilisababisha hali ya kusikitisha na ya kuhuzunisha kwa matukio ya kutisha ya watoto walioungua na kukatwa viungo na vijana waliouawa na kujeruhiwa. Sisi katika Hizb ut Tahrir, tunamuomba Mwenyezi Mungu (swt) msamaha kwa marehemu hao, na tunawaombea nafuu ya haraka waliojeruhiwa. Na tunamuomba Mwenyezi Mungu (swt) awajaalie wahasiriwa hadhi ya mashahidi Peponi kwa mujibu wa bishara njema ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw).

Soma zaidi...

Taasisi zote za Kikoloni, ikiwemo Tume Kuu ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Kibinadamu, ni Ala za kufikia Maslahi ya Marekani; Khilafah pekee kupitia kung'oa Misingi ya Taasisi zote hizi ndio itakayolinda Uislamu, Maslahi ya Watu na Ubwana wa Nchi hii

Licha ya maandamano na wasi wasi wa ngazi zote za wananchi na vyama vya kisiasa, hatimaye serikali ya mpito ya Bangladesh imetia saini makubaliano ya kuanzisha afisi ya taasisi ya Kikoloni yenye ushawishi wa Marekani, Tume Kuu ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa. Uamuzi huu wa serikali umekaribishwa na mashirika ya wanawake yenye chuki dhidi ya Uislamu, ambayo yanashiriki kikamilifu katika usawa wa kijinsia wa Magharibi, utambuzi wa kijamii wa "taaluma" ya kuchukiza ya ukahaba, na kile kinachoitwa haki za binadamu za LGBTQ ikiwa ni pamoja na ushoga unaoangamiza jamii; ilhali wana utata na kukosolewa na ngazi zote za watu kwa sababu hawana sauti katika kuweka haki adilifu na utu wa wanawake, uhuru kutokana na kazi za kikatili, na uboreshaji wa hali ya maisha.

Soma zaidi...

Mauaji ya Kikatili ya Sohag katika eneo la Midford la Mji Mkuu Dhaka, ni Matokeo Yasiyoepukika ya Siasa za Kisekula na za Kiwendawazimu zisizomtambua Mungu

Katika eneo la Mitford la mji mkongwe wa Dhaka, baadhi ya viongozi wa eneo la Jubo Dal, wakiongozwa na chama kikuu cha kisekula cha kisiasa nchini humu BNP, walimuua kikatili mfanyibiashara wa vyuma vichakavu aitwaye Sohag (39) kwa kumdunga kisu na kumpiga na jiwe kubwa mfululizo kwa kukataa kulipa pesa za ulaghai. Walioshuhudia walisema kwamba wahalifu hao hawakuishia kumuua tu, bali waliendelea kuonyesha unyama kwenye mwili mfu wa Sohag hata baada ya kifo chake kuthibitishwa. Mwili uliojaa damu, ulioganda uliachwa katikati ya barabara na wauaji wakasimama juu ya mwili huo huku wakisherehekea kiwendawazimu.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Bangladesh Iliandaa Maandamano na Matembezi ya kupinga Uhamishaji wa India wa Waislamu hadi Bangladesh kwa Mtutu wa Bunduki

Hizb ut Tahrir / Wilayah Bangladesh, iliandaa maandamano na matembezi leo (Ijumaa, 4 Julai 2025) baada ya swala ya Ijumaa katika misikiti mbalimbali ya Dhaka na Chittagong kupinga uhamishaji unaoendelea wa India wa Waislamu hadi Bangladesh kwa mtutu wa bunduki. Wanachama mbalimbali wa Hizb ut Tahrir walitoa hotuba katika maandamano hayo ambayo yalimalizika sambamba na matembezi.

Soma zaidi...

Uhamishaji wa Dola ya Hindutva ya India wa Waislamu hadi Bangladesh kwa Mtutu wa Bunduki ni Uadui wa Wazi kwa Waislamu kama ule wa Umbile Haramu la Kiyahudi

Serikali ya Hindutva ya Modi inaendelea kuongeza kiwango cha ukandamizaji na mateso, ikiwa ni pamoja na kubomoa nyumba za Waislamu wa India na kuwapeleka uhamisho kwa nguvu usio wa haki. Kupitia hili kimsingi wanafuata nyayo za dola haramu ya Kiyahudi ‘Israel’. Hivi karibuni, hata wanawatendea Waislamu wa India kama wanyama kwa kuwaita wahamiaji haramu na kuwarudisha mamia yao nchini Bangladesh kwa mtutu wa bunduki, wakipuuza kile kinachoitwa michakato yao ya kisheria ya kitaifa na kimataifa. "Walitutendea kama wanyama," alisema mwanamke mmoja anayeitwa Rahima Khatun. "Tulipinga kwamba sisi ni Wahindi, kwa nini tuingie Bangladesh? Lakini walituelekezea bunduki na kutishia, 'Ikiwa hamtakwenda kwa huko, tutakupigeni risasi.' Baada ya kusikia milio minne ya risasi kutoka upande wa India, tuliogopa sana na haraka tukavuka mpaka kwa miguu". [Ripoti ya FP].

Soma zaidi...

Ni kutokana na Usaliti wa Watawala Vibaraka wa Ulimwengu wa Kiislamu ambapo Wakatili Wawili wa Amerika - Umbile la Kiyahudi katika Ardhi za Kiarabu na India ya Hindutva huko Asia Kusini - wanaonyesha Kusubutu kwao Kukiuka Ubwana wa Ardhi za Kiislamu

Hizb ut Tahrir / Wilayah Bangladesh, leo (Juni 20, 2025) Ijumaa baada ya swala ya Ijumaa, iliandaa maandamano katika misikiti mbalimbali ya Dhaka na Chittagong kupinga kuendelea kwa mauaji ya halaiki huko Gaza ikiwa ni pamoja na kuzuiliwa kwa chakula na shambulizi dhidi ya Iran na umbile nyakuzi la kiyahudi.

Soma zaidi...

Mkataba wa Yunus-Tarique wa London ni Jaribio la Kudumisha Utawala wa Marekani na Mfumo wao Kandamizi wa Kisekula wa Kibepari

Mnmo tarehe 13 Juni 2025, mkuu wa serikali ya mpito Dkt. Yunus, akiwa amkeketi jijini London, amewakatisha tamaa wananchi kwa kufanya maridhiano ya kisiasa na Tarique Rahman, kaimu mwenyekiti wa BNP (Bangladesh Nationalist Party) kwa sababu watu wa nchi hii hawajasahau historia ya utawala mbaya na ufisadi wa matabaka tawala ya BNP. Kwa hakika, maridhiano haya ya kisiasa ya Yunus-Tarique na kugawanya madaraka ni sehemu ya mpango wa Marekani, ambao kupitia kwao wataweza kutekeleza miradi ya kikoloni. Mumeshuhudia kwamba waliokuwa mabalozi wa Marekani Dan Mozena, Bernicat na Peter Hass, wote wamekaribisha maridhiano haya na kuonesha kuridhika, na kwa mujibu wa taarifa za habari, BNP pia imependekeza kumfanya Dkt. Yunus kuwa rais. Kupitia kuanguka kwa dhalimu Hasina, watu wa nchi hii walionyesha nia yao ya kutaka kuwa huru kutokana na mfumo dhalimu wa kibepari na kutawaliwa na Wakoloni makafiri wa Magharibi. Aina hii ya maridhiano si lolote bali ni usaliti kwa watu wa nchi hii.

Soma zaidi...

Serikali ya Muda Inatengwa na Wananchi kwa sababu ya Utiifu wao kwa Amerika; kwa upande mwingine, Msimamo wa Jeshi letu katika Kupendelea Ubwana wa Nchi kwenye Masuala ya 'Mkondo' na 'Bandari' ni Dhihirisho la Matarajio ya Watu

Huku serikali ya mpito, ikiwapuuza Waislamu wa Rohingya na ubwana wa nchi hiyo, inatamani sana kupeana 'mkondo' kwa maslahi ya kisiasa ya kijiografia ya Amerika na kukabidhi shughuli za 'New Mooring Container Terminal' kwa kampuni yenye ushawishi wa Marekani "DP World", msimamo mkali wa jeshi letu kuunga mkono ubwana wa nchi umesifiwa na watu wengi.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu