Al Waqiyah TV: Wito kwa Waislamu Wote, Na kwa Watu wa Ash-Sham Hasa!
- Imepeperushwa katika Al-Waqiyah TV
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Wito kwa Waislamu Wote, Na kwa Watu wa Ash-Sham Hasa!
Wito kwa Waislamu Wote, Na kwa Watu wa Ash-Sham Hasa!
Asharq Al-Awsat ilichapishwa mnamo tarehe 8 Disemba 2024: (Utawala wa Assad umeanguka: Upinzani wa Syria umetangaza leo, Jumapili, kwamba umeikomboa Damascus na kuupindua utawala wa miaka 24 wa Rais Bashar al-Assad. Taarifa ya upinzani kwenye televisheni ya taifa ilisomeka: “Sifa zote ni za Mwenyezi Mungu, mji wa Damascus umekombolewa na dhalimu Bashar al-Assad amepinduliwa.” Upinzani uliongeza kuwa wafungwa wote wameachiliwa huru.)
Ripoti kuhusu jibu la swali lililotolewa na Amiri wa Hizb ut Tahrir, mwanachuoni mkubwa Ata bin Khalil Abu Al-Rashtah, Mwenyezi Mungu amhifadhi, kuhusu matukio ya Syria na kuanguka kwa utawala wa Assad.
Marekani, Kupitia Usitishwa Vita, inafikia Mambo Mawili Makuu kwa Uadui wa Kiyahudi...
Mnamo tarehe 27 Novemba 2024, usitishaji vita ulitangazwa katika upande wa Lebanon kati ya umbile la Kiyahudi na Hezbollah. Moja ya masharti yake ilikuwa kwamba umbile la Kiyahudi lingeondoa jeshi lake linalovamia kutoka kusini mwa Lebanon ndani ya miezi miwili, huku Hezbollah ingerudisha nyuma majeshi yake kaskazini mwa Mto Litani. Makubaliano hayo pia yalivipa vikosi vya Kiyahudi uhuru wa kutembea kusini endapo chama hicho kitakiuka makubaliano hayo, sambamba na kuendelea na safari za ndege za adui katika anga ya Lebanon kwa ajili ya uchunguzi na ujasusi.
Je, hakuna miongoni mwenu Abdul-Hamid, mlinzi wa Palestina kutokana na Mayahudi… ambaye alimrudisha mwakilishi wao akiwa amekata tamaa na kushindwa, bila kupata chochote, na akamfundisha somo la hekima, akisema: “Siwezi kupeana hata shubiri moja ya ardhi ya Palestina?, kwani sio mali yangu, bali ni mali ya Ummah wa Kiislamu. Watu wangu waliipigania ardhi hii na kuinywesha kwa damu yao… Mayahudi nawabakie na mamilioni yao, kwani ikiwa Dola ya Khilafah itasambaratika siku moja, basi hapo wanaweza kuichukua Palestina bila thamani yoyote, lakini maadamu niko hai, hilo halitafanyika…”?
Mwaka mmoja umepita tangu Kimbunga cha Gaza, ambacho kimetikisa misingi ya hadhara ya Magharibi na kuponda ponda simulizi ya jeshi lisiloweza kushindwa. Mwaka mmoja wa uchinjaji na mauaji ya halaiki ya watu wa Gaza yametekelezwa na nchi za Magharibi zenye chuki na zingali zinaendelea kutekeleza kwa kulitumia umbile nyakuzi. Mwaka mzima wa kula njama na kufanya biashara ya umwagaji damu ambayo watawala wa Waislamu wamegeuka kuwa waovu, na kuwaongezea fedheha.
Enyi askari katika ardhi za Waislamu: Je, hakuna miongoni mwenu mwenye hekima? Ambaye anawaongoza askari, hasa kutoka katika nchi ya Misri (Kinanah), Ash-Sham na ardhi ya Al-Fatih, ili majeshi yaliyosalia yamfuate, yakiimba Allahu Akbar, ili Ummah ufuate Takbira hizo nyuma yao kwa ushindi wa Mwenyezi Mungu (swt)?
Al Waqiyah TV: Enyi Watawala katika Nchi za Waislamu ... Je, Hamuoni Aibu?!