Jumanne, 19 Jumada al-thani 1447 | 2025/12/09
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Mvua ni Baraka na Rehema, lakini bila Uchungaji imekuwa ni Laana!

Ni huzuni na pia inasikitisha kwamba msimu wa mvua hauji kwa ghafla, bali ni kipindi cha taarifa ambacho hurudiwa kila mwaka. Kinachoshangaza zaidi ni kwamba vituo vingi vya uchunguzi wa hali ya hewa vilionya kuhusu mvua kubwa, lakini asasi za serikali hazikuchukua hatua yoyote kuzuia madhara yake, ambayo yalikuwa mabaya zaidi kwa vijiji vya Jimbo la Mto Nile, mashariki mwa Sudan na hata Kordofan, miongoni mwa kwengine.

Soma zaidi...

Wilaya ya Al-Arish Mina, Warraq Mpya Kuwahamisha Wakaazi wake: Uwekezaji wa Lazima au Uhalifu wa Uhamishaji?

Siku hizi, mji wa Al-Arish unashuhudia sura mpya ya mateso wanayopata wananchi wa Misri mikononi mwa utawala unaowaona watu kuwa kikwazo tu kwa mipango yake ya uwekezaji na miradi yenye faida. Baada ya kimya cha miaka mingi na ahadi za uwongo kwamba wakaazi wa wilaya ya Mina kwamba hawatadhurika, watu walishangazwa kukuta matingatinga ya serikali yakiregea kubomoa nyumba na kung’oa wakao yao, bila kujali utakatifu wa nyumba, utu, au haki za watu, ambazo Mwenyezi Mungu (swt) amewapa katika ardhi na mali zao.

Soma zaidi...

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Wanamtembelea Mkuu wa Chama cha Democratic Unionist mjini Al-Obeid

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan, ukiongozwa na Ustadh Al-Nazir Muhammad Hussein - Mjumbe wa Baraza la Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Sudan - akifuatana na Ustadh Issam al-Din Abdul Qadir, walimtembelea Ustadh Khalid Hussein, Mkuu wa Chama cha Democratic Unionist, katika afisi yake katika mji wa Al-Obeid, mnamo Jumanne 3 Rabi’ al-Awwal sawia na tarehe 26 Agosti 2025 M, kama sehemu ya kampeni iliyoandaliwa na Hizb ili kutibua mpango wa kuitenganisha Darfur.

Soma zaidi...

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Waitembelea Idara ya Muongozo na Ushauri katika Jimbo la White Nile

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan – Mji wa Rabak, White Nile, uliitembelea Idara ya Muongozo na Ushauri mnamo Jumapili, 1 Rabi' al-Awwal 1447 H sawia na tarehe 24 Agosti 2025. Ujumbe huo ulikutana na mkuu wa Sekretarieti katika Jimbo la White Nile, Sheikh Abdul Mubara Mahmoud Al-Mahmoud. Ujumbe huo uliongozwa na Dkt. Ahmed Muhammad Fadl Al-Sayyid, mwanachama wa Hizb ut Tahrir, na alifuatana na Ustadh Faisal Madani, mwanachama wa Hizb ut Tahrir.

Soma zaidi...

“Israel” kama Mradi wa Kikoloni – na Uholanzi kama Nguzo Yake

Kuondolewa kwa Mkataba wa Kijamii wa Nieuw (BMT) kutoka kwa serikali kuliwasilishwa haraka kwenye vyombo vya habari kama hatua ya kikanuni. Kana kwamba upande huo hatimaye ulivunja sera kwa sababu ya mateso ya kutisha ya Wapalestina mjini Gaza. Lakini hiyo ni dhana potofu. Kuondoka kwao sio dhihirisho la chukizo la kimaadili, bali ni hesabu za kisiasa. Haitoi BMT nje ya mradi wa kikoloni unaoitwa “Israel”, lakini inaonyesha jinsi wao pia wamenaswa kwa kina ndani yake.

Soma zaidi...

Hali Baada ya Mvua na Mafuriko kwa Mara Nyingine Tena Imeweka Wazi Kuwa Waislamu Wanahitaji Mchungaji Khalifah

Tangu Juni 26, mafuriko katika maeneo mbalimbali ya Khyber Pakhtunkhwa, Punjab, na Karachi yamesababisha vifo vya zaidi ya watu 650 na kujeruhi zaidi ya elfu moja. Maelfu ya nyumba zimesombwa na maji, pamoja na akiba za maisha yote za watu, mali za nyumbani, na magari. Dada na mabinti zetu—ishara za staha na heshima—wamenyimwa nyumba na faragha zao, wakilazimishwa kuishi chini ya anga wazi.

Soma zaidi...

Usaliti Mpya: Mamlaka ya Lebanon Yamwachilia Huru Mmoja wa Wafungwa Wanaohusishwa na umbile la Kiyahudi!

Leo, Alhamisi, tarehe 21/8/2025, mamlaka ya Lebanon ilimwachia huru ghafla Saleh Abu Hussein, ambaye ni mmoja wa washirika wa umbile la Kiyahudi, bila kubadilishana na yeyote! Na wakamkabidhi kwa umbile hilo kililokuwa mstari wa mbele wa ukaliaji kimabavu wa Palestina mjini Naqoura!

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu