Jumatano, 15 Ramadan 1447 | 2026/03/04
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Wanawake wa Kashmiri Walibakwa na Kuteswa na Uvamizi wa Dola ya India Tangu 1947

Wakati wa Kikao cha 60 cha Baraza la Haki za Kibinadamu la Umoja wa Mataifa (UNHRC) mwaka huu, Kikao cha Kimataifa kisicho cha Kiserikali kilifanyika kuhusu Haki za Kiuchumi, Kijamii na Kitamaduni za Wanawake, kilichoandaliwa na OCAPROCE International chini ya kichwa, “Wanawake kwa ajili ya Kukuuza na Kulinda Turathi ya Kitamaduni na Ujenzi wa Amani Endelevu ifikapo 2030,” ambapo mwakilishi wa wanawake wa Kashmir Dkt. Shugufta, aliangazia masaibu ya wanawake wa Kashmir mikononi mwa gaidi amvamizi, vikosi vya jeshi la India. Alisema, “Ninasimama mbele yenu leo ​​kwa sauti inayobeba maumivu ya wanawake wengi walionyamazishwa kutoka bonde la Jammu na Kashmir Inayokaliwa Kimabavu Kinyume cha Sheria.

Soma zaidi...

Kitengo cha Wanawake katika Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir Chahitimisha Kampeni yake ya Kimataifa: “Vita vya Sudan: Hadithi ya Ukoloni, Usaliti na Udanganyifu”

Katika kipindi cha miezi miwili iliyopita, Kitengo cha Wanawake katika Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir kimeendesha kampeni ya kimataifa ya kuinua ufahamu wa kimataifa na kuleta muanga wa kimataifa kuhusu mgogoro wa kutisha wa kibinadamu uliosababishwa na mzozo nchini Sudan ambao umekuwa ukiendelea kwa miaka mitatu na nusu sasa. Mzozo huu usio na maana, kati ya Vikosi vya Wanajeshi wa Sudan (SAF) vinavyoongozwa na Jenerali Abdel Fattah al-Burhan, na Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) vinavyoongozwa na Mohamed Hamdan Dagalo (“Hemedti”), umesifiwa kama “Vita Vilivyosahaulika” kutokana na kutopokea uangaziaji wa vyombo vya habari na uangalizi wa kimataifa unaostahili.

Soma zaidi...

Kimbunga cha Al-Aqsa kiko Hai na Kinaendelea

Operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa haikuwa tukio la muda mfupi ambalo lilimalizika kwa makubaliano ya mhalifu Trump na dola ya kikafiri nyuma yake, Marekani, muungaji mkono rasmi wa umbile la Kiyahudi. Badala yake, Kimbunga cha Al-Aqsa kilikuwa ni cheche iliyowasha moto ndani ya nyoyo za Waislamu, na kuzifungua akili na nyoyo zao. Waliona unyonge na uovu wa watawala wao wasaliti, na wakatambua unafiki wa wale wanaodai kuwa ni na ubinadamu, na wanaotetea haki za wanawake na watoto. Wakawa na hakika kwamba sheria za kimataifa, na mikataba si chochote ila ni silaha inayotumiwa na makafiri, dhidi ya Uislamu na Waislamu.

Soma zaidi...

Maadhimisho ya Mwaka wa Pili wa Operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa Matunda Yaliyonyunyiziwa kwa Damu Safi

Tarehe 7 Oktoba iliadhimisha mwaka wa pili wa operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa. Miaka miwili kamili imepita tangu umbile nyakuzi kulenga watu wetu mjini Gaza, likiwafungulia mpangilio wa kuua, kuhamisha, na njaa, na kutumia viwango vya juu vya ushenzi na ukatili dhidi yao. Kwa hivyo ni nini kimebadilika kwa vita hivi vya dhulma?!

Soma zaidi...

Kongamano la Sharm El-Sheikh Ni Kutangaza Ushindi Juu ya Ummah, Kumakinisha Utiifu, na Kuimarisha Ukaliaji wa Kimabavu

Baada ya Trump kutangaza ushindi yeye na mfuasi wake, umbile la Kiyahudi, walioupata katika hotuba yake mbele ya Knesset. Ushindi huu ulipatikana dhidi ya raia wasio na silaha, wakiwemo wanawake, watoto, na wazee, pamoja na miti na mawe, Muuaji wa Gaza alielekea kwenye kongamano hilo liliopangwa na kibaraka wake nchini Misri, Sisi, ambapo aliwaalika wale wote waliokula njama dhidi ya ardhi iliyobarikiwa.

Soma zaidi...

Kuongezeka kwa Umwagaji damu kwenye Mpaka wa Pakistan na Afghanistan na Kushindwa kwa Pande zote mbili Kushikamana na Hukmu ya Mwenyezi Mungu

Mbali na sera ya “kujizuia” iliyotabanniwa na serikali za sasa za Pakistan na Afghanistan kwa maadui wa Umma – Mayahudi, Mabaniani, na Waamerika – Pakistan pamoja na Afghanistan zilitangaza kwamba makumi ya wanajeshi kutoka kila upande walikuwa wameuawa katika mapigano ambayo yalizuka kwenye mpaka wao wa pamoja. Makabiliano hayo yalianza mnamo Jumamosi jioni kwa operesheni iliyoanzishwa na vikosi vya Taliban, na kusababisha Islamabad kuapa kutoa jibu kali. Kabul, kwa upande wake, ilitangaza kuwa vikosi vyake vilifanya operesheni dhidi ya vikosi vya usalama vya Pakistan ili kulipiza kisasi kwa ukiukaji wa mara kwa mara na uvamizi wa anga unaofanywa na jeshi la Pakistan katika eneo la Afghanistan.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu