Jumapili, 17 Jumada al-thani 1447 | 2025/12/07
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Trump, Kupitia Azimio la Umoja wa Mataifa na kwa Msaada wa Watawala Waislamu, Anajiandaa Kuiweka Gaza na Eneo la Ash-Sham Chini ya Udhibiti wa Moja kwa Moja wa Kikoloni

Wakati wowote Amerika inaposhindwa kufanya jambo peke yake, hutumia mwavuli dhalimu wa Umoja wa Mataifa. Azimio la kishetani nambari 2803, lililoundwa kukandamiza upinzani wa Palestina, ni hila ya hivi karibuni ya Farauni wa leo, Trump. Kulingana na azimio hili ovu lililopitishwa tarehe 17 Novemba, ambalo serikali ya Pakistan ililipigia kura kwa aibu chini ya amri ya Trump, utawala wa Gaza utawekwa chini ya “Bodi ya Amani (BoP),” inayoongozwa binafsi na Farauni Trump. Azimio hilo hilo lililopitishwa tarehe 17 Novemba linatoa mamlaka kwa “Kikosi cha Kimataifa cha Utulivu,” kinachojumuisha wanajeshi kutoka nchi za Kiislamu, kulinda umbile la Kiyahudi na kupokonya silaha upinzani wa Palestina. Kivitendo, hili litakigeuza kuwa “Kikosi cha Ulinzi cha Israel” kinachofanya kazi chini ya amri ya Trump. “Bodi hii ya Amani (BoP)” na muundo wake wa usalama unaoambatana nayo itasimamia Gaza hadi tarehe 31 Disemba 2027, pamoja na uwezekano wa kuongezwa muda.

Soma zaidi...

Pakistan, Nchi Safi, Haiwakaribishi Wala Haiwasalimu Vizazi vya Khiyana vya Wasaliti

Baada ya kimya cha wafu makaburini cha serikali za vibaraka zinazobebesha mzigo ardhi za Waislamu, kuhusu mauaji ya Kiyahudi mjini Gaza kwa zaidi ya miaka miwili, vibaraka wa Amerika na Uingereza, washirika wa Mayahudi, walianza kuchukua hatua na kuwa wachangamfu katika kutekeleza mpango wa Trump wa kufilisi kile kilichobaki cha upinzani huko Palestina, kukandamiza na kuua watu mjini Gaza, na kubomoa kile ambacho Mayahudi hawakubomoa cha mawe. “Jenerali anayependwa zaidi wa Trump” Asim Munir alitembelea Jordan mnamo 26 Oktoba, na kwa badali yake, mnamo 16 Novemba 2025, Mfalme Abdullah II bin Al-Hussein, Mfalme wa Ufalme wa Hashimiya wa Jordan na Kamanda Mkuu wa Vikosi vya Wanajeshi wa Jordan, alitembelea Pakistan, akifuatana na binti yake Salma binti Abdullah II bin Al-Hussein, na ujumbe wa maafisa wa kiraia na kijeshi wa Jordan.

Soma zaidi...

Vikosi vya Pakistan Lazima Vitumwe Kuikomboa Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina, Sio Kutimiza Ndoto za Adui wa Mwenyezi Mungu (swt), Trump, na Mayahudi!

Kutumwa kwa vikosi vya jeshi la Pakistani Gaza kuwanusuru watu wake na kupigana na Mayahudi ambao wameendelea na operesheni ya mauaji ya halaiki huko, tangu tarehe 7 Oktoba 2023 hakukujadiliwa kamwe, kwa kisingizio kwamba Gaza iko mbali, na kwamba wajibu wa Sharia wa kuinusuru unawaangukia wale walio karibu zaidi. Lakini mara tu bwana wa serikali ya Pakistan na adui wa Mwenyezi Mungu (swt), Trump, alipoamuru serikali hii kutuma vikosi ili kufikia ndoto zake mjini Gaza, ghafla Pakistan ikawa nchi jirani na Gaza, na vikosi vya jeshi la Pakistan vimewekwa tayari kufanya operesheni za kijeshi nje ya mipaka ya kitaifa ya Pakistan. Hivyo uongo wa serikali hii ulifichuliwa kuhusu kutoweza kwake kutuma vikosi vya jeshi kuwanusuru watu wetu mjini Gaza.

Soma zaidi...

Mahouthi Wawakamata Mashababu wa Hizb ut Tahrir kwa Kufichua Mkataba wa Trump!

Mnamo Ijumaa, 21/11/2025, kundi la Mahouthi katika Jimbo la Ibb liliwakamata wanachama wawili wa Hizb ut Tahrir, ndugu: Osama Muhammad Mas’ad Al-Wurafi (umri wa miaka 19) na Ibrahim Muhammad Mas’ad Al-Wurafi (umri wa miaka 15) kufuatia usambazaji wao wa toleo lililotolewa na Hizb ut Tahrir lenye kichwa: “Trump Anawaongoza Wafuasi Wake miongoni mwa Watawala katika Ardhi za Waislamu Kwenye Mkataba wa Fedheha na Aibu, Wakiinamisha Vichwa Vyao Nyuma Yake kwa Kuiweka Gaza Hashem chini ya Usimamizi na Ukoloni!” Toleo hili lilisambazwa nchini Yemen na nchi nyingi za Waislamu.

Soma zaidi...

Mauaji Mapya Yatekelezwa na Umbile Halifu la Kiyahudi katika Kambi ya Ain Al-Hilweh!

Katika muktadha wa kile ambacho Amerika inaendesha katika suala la amani na uhalalishaji mahusiano nchini Lebanon na eneo hili—ambapo kiuhalisia ni kusalim amri na kujisalimisha—umbile halifu nyakuzi la Kiyahudi, pamoja na silaha za Marekani, risasi za Ulaya, mikono ya Kiyahudi, na ushirika rasmi wa Waarabu, lililipua uwanja wa michezo na klabu ya michezo katika kambi ya Ain al-Hilweh katika mji wa Sidon kusini mwa Lebanon mnamo Jumanne, 18/11/2025. Mashahidi kumi na tano waliauwawa katika shambulizi hili la kikatili, na makumi ya watoto na raia walijeruhiwa, katika shambulizi baya linalothibitisha uhalifu wa umbile la Kiyahudi na uadui wake dhidi ya Waislamu.

Soma zaidi...

Kauli za Patriarch Bechara Al-Rahi Kuhusu Wakristo katika Eneo Hili Mshikamano wa Kudumu kwa Fahamu ya Marekani na Kimagharibi ya “Walio wachache”, iliyo ngeni kwa Watu wa Eneo Hili na Historia Yao!

Katika mahojiano yake na chaneli ya Lebanon Al-Jadeed katika kipindi cha “Huyu ni Mimi” na mwandishi wa habari Samar Abu Khaleel, kauli za Patriarch Bechara Al-Rahi zinaambatana na ziara ya Papa Leo XIV katika eneo hili, ikiwa ni pamoja na Lebanon, hasa kuhusu suala la kubadilisha utawala wa Syria na kauli yake: “Wakristo wanaondoka Syria leo kwa sababu dola iliyopo ni dola ya Kiislamu! Ingawa haikuwa hivyo wakati wa utawala uliopita...” Na msimamo huu ni uthibitisho wa msimamo uliopita wa Patriarch mwenyewe; ambapo alisema mwaka wa 2011 wakati wa ziara yake nchini Ufaransa chini ya Sarkozy: “Kukiri kwamba makosa na ukiukwaji wa sheria uliotokea nchini Syria hakubatilishi ukweli kwamba Rais Bashar Al-Assad alikuwa ameanza mageuzi, na angepaswa kupewa nafasi”!

Soma zaidi...

Mwaliko wa Kuhudhuria Muhadhara wa Kisiasa

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan inafuraha kuwaalika wataalamu wa vyombo vya habari, wanasiasa, na wale wote wanaopenda masuala ya umma kuhudhuria na kushiriki katika muhadhara mpya ya Kikao cha Kisiasa, ambao utawasilishwa na Ustadh Ibrahim Mushrif, mwanachama wa Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan, wenye kichwa: Mzozo wa Kikoloni barani Afrika - Sudan kama Mfano

Soma zaidi...

Wanamgambo ni Tishio la Usalama kwa Umbo la Serikali, na Uwepo Wao ni Ukiukaji wa Sharia

Mapigano ya silaha yalitokea katika mji wa Dongola, mji mkuu wa Jimbo la Kaskazini, jioni ya Ijumaa, 21/11/2025, kati ya vikosi vya jeshi la Sudan na kikundi chenye silaha kinachojulikana kama Awlad Gamri, kaskazini mwa kituo cha usafiri wa miji. Kulingana na kile kilichoripotiwa katika habari, kiongozi wa kikundi hicho, anayeitwa Al-Tom Gamri, alijeruhiwa na kupelekwa hospitalini, na kuna habari za kuuawa kwa mlinzi wake binafsi.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Uturuki: Kongamano la Antalya: “Usuli wa Amani na Mustakabali wa Gaza”

Katika kukabiliana na mauaji ya kikatili yanayoendelea (mauaji ya halaiki) yanayofanywa na umbile halifu la Kizayuni dhidi ya Waislamu wasio na ulinzi katika Ukanda wa Gaza kwa zaidi ya miaka miwili, ambayo yamesababisha kuuawa shahidi, kujeruhiwa, na kutoweka kwa Waislamu zaidi ya 220,000 hadi sasa, Hizb ut-Tahrir / Wilayah Uturuki iliandaa kongamano la pamoja jijini Antalya lenye kichwa: “Usuli wa Amani na Mustakabali wa Gaza.”

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu