Rais wa Slovenia Hajui Historia, au Anaipuuza!
- Imepeperushwa katika Afisi Kuu ya Habari
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Hii ilikuwa katika mahojiano na Kituo cha Al Jazeera mnamo 9/11/2025, ambayo kituo kilitangaza kikamilifu asubuhi ya 10/11/2025. Kutoka ardhi ya Waislamu huko Qatar, Rais wa Slovenia, Nataša Pirc Musar, anasema: “Israel ina haki ya kuwa na dola.” Swali linaloelekezwa kwa rais ni: Ni nani aliyelipa umbile hili haramu la Kiyahudi haki hii? Na je, kuna mtu yeyote anayesoma historia na hajui jinsi umbile hili lemavu lilivyoanzishwa katika ardhi iliyobarikiwa ya Palestina? Je, mauaji ya Mayahudi dhidi ya Waislamu, watu wa Palestina, yanaondoka akilini mwa msomaji yeyote adilifu wa historia? Umbile hili lemavu lilisimamishwaje juu ya mafuvu na maiti za watu wengi wa Palestina?



