Jumapili, 23 Safar 1447 | 2025/08/17
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Ewe Hamasa ya Uislamu ndani ya Umma wa Muhammad (saw) Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw) amesema: “Si Muumini anayelala ameshiba na hali jirani yake ana njaa.”

Miti na mawe yamelia kutokana na hofu iliyotusibu. Vifua vyetu vinatoa damu na maumivu, watoto wetu wanasisimka kutokana na njaa na kiu, wanawake wetu wanalia ili kuchochea wivu wa ulinzi wa waumini. Asiyeuawa kwa kupigwa mabomu hufa kwa njaa na kiu. Lakini maumivu ya usaliti ni mazito juu yetu kuliko milipuko ya mabomu, njaa, na kiu. Kaka na dada zenu mjini Gaza wanatangatanga bila malengo, bila makaazi, sauti zao zimenyamazishwa na udhaifu ulioletwa na njaa na kiu, baada ya kutoweka matumaini yote kwamba yeyote isipokuwa Mwenyezi Mungu atakuja kuwasaidia. Wanapiga kelele: Uko wapi Umma wa Uislamu? Iko wapi hamasa ya Dini? Uko wapi msaada wa Waumini?

Soma zaidi...

Taasisi zote za Kikoloni, ikiwemo Tume Kuu ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Kibinadamu, ni Ala za kufikia Maslahi ya Marekani; Khilafah pekee kupitia kung'oa Misingi ya Taasisi zote hizi ndio itakayolinda Uislamu, Maslahi ya Watu na Ubwana wa Nchi hii

Licha ya maandamano na wasi wasi wa ngazi zote za wananchi na vyama vya kisiasa, hatimaye serikali ya mpito ya Bangladesh imetia saini makubaliano ya kuanzisha afisi ya taasisi ya Kikoloni yenye ushawishi wa Marekani, Tume Kuu ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa. Uamuzi huu wa serikali umekaribishwa na mashirika ya wanawake yenye chuki dhidi ya Uislamu, ambayo yanashiriki kikamilifu katika usawa wa kijinsia wa Magharibi, utambuzi wa kijamii wa "taaluma" ya kuchukiza ya ukahaba, na kile kinachoitwa haki za binadamu za LGBTQ ikiwa ni pamoja na ushoga unaoangamiza jamii; ilhali wana utata na kukosolewa na ngazi zote za watu kwa sababu hawana sauti katika kuweka haki adilifu na utu wa wanawake, uhuru kutokana na kazi za kikatili, na uboreshaji wa hali ya maisha.

Soma zaidi...

Majanga na Maafa ni Matokeo ya Kimaumbile ya Kukosekana Dola yenye Kujali

Katika msururu wa ajali za mara kwa mara na moto wa kutisha-hasa ule moto wa ukumbi wa harusi wa mwaka 2023 huko Ninawi, ambao uligharimu maisha ya zaidi ya watu 120 na kujeruhi 200; moto wa mwaka 2021 katika Hospitali ya Al-Hussein huko Dhi Qar, ambao uliua zaidi ya watu 92; na moto wa mwaka 2021 wa kituo cha utengaji wagonjwa wa COVID-19 katika Hospitali ya Ibn Al-Khatib jijini Baghdad, ambao ulisababisha vifo vya watu 82-unakuja msiba mwengine tena wa kutisha. Moto mkubwa ulizuka katika soko kuu la Kut jioni ya Jumatano, 16 Julai 2025. Wizara ya Mambo ya Ndani ya Iraq ilithibitisha kuwa moto huo, ambao ulizuka ndani ya jengo la biashara la ghorofa tano katikati mwa mji wa Kut, uliwaua watu 61, ikiwa ni pamoja na miili 14 iliyoungua ambayo bado haijatambuliwa. Waathiriwa wengi walikufa kutokana na kuvuta moshi. Wizara hiyo iliongeza kuwa jengo hilo ambalo lilikuwa na mkahawa na kituo cha biashara, lilikuwa limefunguliwa kwa siku saba pekee.

Soma zaidi...

Matukio ya Umwagaji damu huko Sweida Yafichua Hatari za Makundi Yenye Uhusiano wa Kigeni Uhalalishaji Mahusiano ni Jinai Inayohujumu Miaka 14 ya Muhanga wa Mapinduzi

Kufuatia siku kadhaa za mapigano makali yaliyogharimu maisha ya mamia ya ndugu zetu waliokufa shahidi, Wizara ya Ulinzi ghafla na kwa mshtuko ilitangaza Jumatano kuwa ni siku ya kuanza kujiondoa kwa jeshi la Syria katika mji wa Sweida. Haya yanajiri baada ya wito wa Marekani wa kuondoa vikosi vya serikali katika jimbo hilo na msururu wa mashambulizi makali ya anga yaliyofanywa na umbile la Kiyahudi mjini Damascus siku ya Jumatano, Julai 16, 2025, yakilenga jengo la Jeshi, Wizara ya Ulinzi na maeneo jirani ya Kasri la Rais. Mashambulizi ya awali yalikuwa yamepiga maeneo mengi viungani mwa Damascus, Daraa na Sweida, yakilenga maeneo ya kijeshi na misafara ya jeshi la Syria na vikosi jumla vya usalama vilivyokuwa vikielekea Sweida, na kusababisha idadi kubwa ya mashahidi na majeruhi.

Soma zaidi...

Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir: Kitengo cha Wanawake “Kampeni ya Kimataifa - Vita vya Sudan: Hadithi ya Ukoloni, Usaliti na Udanganyifu”

Kitengo cha Wanawake katika Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir Kimezindua kampeni ya kimataifa kuangazia maafa yanayozidi kuwa mabaya ya kibinadamu yanayowakabili Waislamu wa Sudan. Kampeni hii pia itashughulikia: siasa na ajenda zilizofichwa nyuma ya mzozo huu.

Soma zaidi...

Kitengo cha Wanawake katika Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir Chazindua Kampeni ya Kimataifa “Vita vya Sudan: Hadithi ya Ukoloni, Usaliti na Udanganyifu”

Mgogoro wa kikatili nchini Sudan kati ya Wanajeshi wa Sudan (SAF) wanaoongozwa na mtawala mkuu wa Sudan, Jenerali Abdel Fattah al-Burhan, na Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF) kinachoongozwa na Mohamed Hamdan Dagalo (Hemedti), ambaye hapo awali alikuwa naibu wa al-Burhan katika Baraza Kuu, sasa umeingia mwaka wake wa tatu, na kusababisha vifo vya maelfu ya raia. Baadhi ya makadirio yanaweka idadi ya waliofariki katika vita hivi vya kipumbavu kufikia 150,000, huku kukiwa na ukatili wa kutisha uliofanywa na pande zote mbili, ikiwa ni pamoja na mauaji ya kinyama, mateso, ubakaji mkubwa na uhalifu mwingine wa kingono dhidi ya wanawake na wasichana. Mauaji ya kikabila pia yameripotiwa, huku jamii nzima zikiteketezwa kwa moto na kuangamizwa, na mauaji ya halaiki katika miji mbalimbali, vijiji na kambi za watu waliokimbia makaazi yao.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Uturuki: Matembezi ya Halaiki ya Kuinusuru Gaza “Kuwahutubia wale Wanaohusika!”

Kwa kuzingatia mauaji ya kikatili (mauaji ya halaiki) ambayo yamekuwa yakiendelea kwa muda wa miezi 21, yanayofanywa na umbile halifu la Kiyahudi dhidi ya Waislamu wasio na ulinzi katika Ukanda wa Gaza, ambayo yamesababisha kuuawa shahidi, kujeruhiwa na kupotezwa kwa zaidi ya wanaume na wanawake 200,000 Waislamu hadi sasa. Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Uturuki iliandaa matembezi makubwa ya halaiki kote nchini Uturuki licha ya serikali ya Uturuki kuyapiga marufuku.

Soma zaidi...

Mkataba wa Biashara na Unyenyekeaji wa Indonesia kwa Maslahi ya Marekani

Rais wa Marekani Donald Trump alitangaza makubaliano ya kibiashara na Indonesia, kupunguza ushuru unaotishiwa wa 32% kwa bidhaa za Indonesia hadi 19%. Kwa upande wake, Indonesia ilijitolea kununua nishati ya Marekani kwa dolari bilioni 15, bidhaa za kilimo kwa dolari bilioni 4.5, na ndege 50 za Boeing, ikiwa ni pamoja na aina ya 777. Trump alidai Marekani itapata ufikiaji kamili wa soko la Indonesia bila kulipa ushuru. Makubaliano hayo yalifuatia vitisho vya ushuru wa juu na yalikamilishwa baada ya mazungumzo na Rais wa Indonesia Prabowo Subianto. Bado haijulikani ni lini upunguzaji wa ushuru na ununuzi utaanza kutekelezeka. Biashara ya Indonesia na Marekani ilifikia karibu dolari bilioni 40 mwaka 2024, na nakisi ya biashara ya bidhaa za Marekani ya takriban dolari bilioni 18.

Soma zaidi...

Idhini ya Marekani sio Kipimo cha Uamuzi wa Kisiasa kwa Umma wa Kiislamu

Mnamo tarehe 17 Julai 2025, Dawn News ilinukuu kutoka Reuters, "Ikulu ya White House mnamo Alhamisi ilisema kwamba hakuna ziara ya Rais wa Marekani Donald Trump iliyopangwa Pakistan "kwa wakati huu" baada ya kuenea kwa taarifa za safari hiyo. Mapema siku hiyo, baadhi ya vituo vya habari vya televisheni vya ndani viliripoti, vikinukuu vyanzo, kwamba Trump alitarajiwa kuzuru Pakistan mwezi Septemba. Chaneli za habari zilisema kwamba Trump pia angetembelea India baada ya kuwasili jijini Islamabad mwezi Septemba. Chaneli hizo baadaye ziliondoa ripoti zao.” [Dawn]

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu