Jumapili, 17 Jumada al-thani 1447 | 2025/12/07
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Gaza Inavuna Mavuno Uchungu ya Baraza la Usalama na Uamuzi wa Baraza la Amani

Siku chache baada ya uamuzi wa Baraza la Usalama, watu wa Gaza walianza kuvuna hasara yake; katika muda usiozidi masaa 24, mashahidi 34—wengi wao wakiwa watoto na wanawake—walikuwa wamepanda daraja hiyo hadi kufikia Alhamisi asubuhi, 20/11/2025, pamoja na makumi ya waliojeruhiwa kutokana na uzito wa njaa na kwenye makucha ya baridi kali. Damu hizi safi zilikuwa maana halisi ya uamuzi ulioipa Amerika usimamizi na mamlaka juu ya Ukanda wa Gaza, ikiruhusu kukata vichwa kama ilivyotaka. Ni uamuzi uliopuuza damu, utajiri, na ardhi za watu wa Palestina katika Ukingo wa Magharibi na kuachilia mkono wa Mayahudi kutumbukia ndani ya damu yetu, ambayo ilienea zaidi ya Gaza hadi Kambi ya Ain al-Hilweh nchini Lebanon.

Soma zaidi...

Abbas, Akizungumza kutoka Pango la Maadui wa Uislamu jijini Paris, Anathibitisha Dori ya Kihalifu ya Mamlaka ya Palestina katika Kutekeleza Sera za Marekani na Mayahudi Zinazolenga Kufuta Kadhia ya Palestina na Kuwakata Watu wa Palestina na Watoto Wa

Katika mkutano kati ya Abbas na Macron jijini Paris mnamo Jumanne, 11 Novemba 2025, ambapo kuundwa kwa kamati ya pamoja ya Ufaransa na Palestina ya kuandika katiba ya dola ya Palestina kulitangazwa (Al Jazeera Mubasher), Abbas anaonekana kupata msukumo kutoka kwa historia ya dola zilizo katika eneo hili zilizopitisha katiba za Magharibi kama msingi wa sheria zao. Wamewachukua Wamagharibi kama mabwana zao, badala ya Mwenyezi Mungu Mtukufu. Abbas hakuweza kufanya chochote ila kugeukia Paris na kuwaomba mabwana zake kuandika katiba ya dola iliyo kwenye karatasi—dola ambayo hawezi kuingia au kutoka bila idhini ya Mayahudi.

Soma zaidi...

Kampeni ya Umbile la Kizayuni katika Ukingo wa Kaskazini Magharibi ni Sehemu ya Mpango wake wa Kuimarisha Makaazi na Kuimarisha Udhibiti wake katika Eneo Hilo. Je, Hakuna Kiongozi Anayeongozwa na Mungu wa Kuikomboa Ardhi Iliyobarikiwa?!

Hawa hapa Mayahudi wakizidi kuwa wakali zaidi katika Ukingo wa Magharibi, wakitangaza “operesheni ya kijeshi” kaskazini mwake, wakibomoa nyumba na kuzigeuza zengine kuwa kambi za kijeshi, wakinyang'anya ardhi, wakikamata kundi la Wapalestina na kuua kundi jengine, wakiharibu mifereji ya maji na kung'oa miti, na operesheni yao ya kijeshi inaenea hadi sehemu iliyobaki ya Ukingo wa Magharibi, katikati yake na kusini yake, na hii inaendana na kile walowezi hao wanachofanya, kwa kuzingatia kutolewa kwa sheria inayowaruhusu kupata mali katika Ukingo wa Magharibi, ambayo ilitanguliwa na kufutiliwa mbali kwa sheria ya kutengwa kaskazini yake.

Soma zaidi...

Enyi Watu wa Sudan, Amerika Inaharakisha Kuvuna Matunda ya Vita vyake nchini Sudan, Kwa hivyo Msiiruhusu Itenganishe Darfur

Wakati wa hotuba yake katika Kikao cha Uwekezaji kati ya Marekani na Saudi Arabia, Rais wa Marekani Donald Trump alisema kwamba Mfalme Mtarajiwa Mohammed bin Salman alikuwa ameomba azimio la mgogoro nchini Sudan, akiongeza kwamba alianza kusoma suala hilo nusu saa tu baada ya maelezo ya Mwanafalme huyo. Trump pia aliandika kwenye tovuti yake ya Kijamii ya Truth kwamba atatumia mamlaka ya urais kusimamisha vita mara moja.

Soma zaidi...

Jibu la Swali: China na Ukombozi Wake Kutoka kwa Mtazamo Wake Mdogo wa Kikanda

 “China inamiliki hisia ya nguvu na mapambano, na kama lengo la China halikufungika tu na kudumisha eneo lake, na kukubali kukabiliana na Amerika kama jibu tu kwa harakati za Amerika kuelekea eneo lake, China haisubutu kupambana na Amerika katika maeneo yao ya ushawishi... na kama isingeanza kutumia ubepari katika nyanja nyingi, haswa katika uchumi... ingekuwa na sauti kubwa kimataifa, na athari yake kwa maslahi ya Amerika ingekuwa na nguvu zaidi. China kwa vyovyote vile ina hisia kali ya nguvu, na inafanya kazi ili kudumisha ubwana wa eneo lake, hata kama iko katika eneo lake...” — Kwa hivyo, je, kizuizi cha China cha mauzo ya nje ya madini adimu ya ardhini kwenda Amerika, kuyauza kwa dhamana za Hazina ya Marekani, kulisasisha jeshi lake, na kujenga jengo kubwa zaidi la kijeshi duniani kusini magharibi mwa Beijing... je, hiki si kiashiria cha ukombozi wa China kutoka kwa mtazamo wake wa kisiasa uliofungika katika eneo lake na upanuzi wa mtazamo huu kushindana na Amerika duniani kote?

Soma zaidi...

Jibu la Swali: Ruwaza ya Marekani ya Kutatua Kadhia ya Cyprus

“Afisi ya rais wa Uturuki ilitangaza mnamo Jumatatu kwamba Rais wa Jamhuri ya Uturuki ya Cyprus Kaskazini, Tufan Erhürman, atatembelea Ankara Alhamisi ijayo, 13/11/2025... Burhanettin Duran, mkuu wa idara ya mawasiliano ya rais wa Uturuki, alisema kwamba ziara ya Erhürman Ankara inakuja kutokana na mwaliko wa Rais Erdoğan, na Duran aliongeza kwamba ziara hiyo itakuwa kituo cha kwanza cha kigeni cha Erhurman... Na mnamo tarehe 19 Oktoba Bodi Kuu ya Uchaguzi ya Uturuki ya Cyprus ilitangaza ushindi wa kiongozi wa Chama cha Republican cha Kituruki, Tufan Erhürman, katika uchaguzi wa rais.” (Shirika la Anadolu, 10/11/2025). Kwa hivyo ni nini kimesababisha maridhiano haya? Ikifahamika kwamba Erhurman, wakati wa kampeni yake ya uchaguzi, alikuwa akitoa wito wa kuunganisha kisiwa hicho, huku Erdogan akitoa wito wa dola mbili? Na je, Amerika iko nyuma ya maridhiano hayo? Na Mwenyezi Mungu akulipe kheri.

Soma zaidi...

Trump Awaongoza Wafuasi wake kutoka kwa Watawala katika Ardhi za Waislamu kwenye Mkataba wa Fedheha na Aibu, Wakiinamisha Vichwa Vyao Nyuma Yake kwa Kuiweka Gaza Hashem chini ya Usimamizi na Ukoloni!

“Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lilipitisha alfajiri ya Jumanne mpango wa Rais wa Marekani Donald Trump kuhusu Ukanda wa Gaza baada ya kuidhinisha rasimu ya azimio lililowasilishwa na Marekani na kuunga mkono mpango wa amani wa Trump katika sekta hiyo, na Rais Trump aliisifu kura ya Baraza la Usalama kuhusu azimio la Gaza kama wakati wa kihistoria...” (BBC, 18/11/2025). Kuhusu Azimio Nambari 2803, lilichapishwa na vyombo vya habari na lilikuwa ni idhini ya mpango wa pointi 20 wa Rais Donald Trump wa kukomesha mzozo mjini Gaza, lililotolewa mnamo tarehe 29 Septemba 2025.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu