Jumatano, 07 Muharram 1447 | 2025/07/02
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Serikali ya Hindutva ya India Inaendelea Kutumia Shirika la Kitaifa la Uchunguzi kwa Kazi yake Chafu

Mnamo tarehe 14 Juni 2025, Shirika  la Kitaifa la Uchunguzi (NIA) lilifanya uvamizi ulioratibiwa katika maeneo matatu huko Bhopal, Madhya Pradesh, na miwili huko Jhalawar, Rajasthan, kuhusiana na kesi ya Hizb ut Tahrir (HuT). Operesheni hiyo ililenga kukusanya ushahidi zaidi dhidi ya HuT. NIA ilidai kuwa uvamizi huu ulisababisha kukamatwa kwa "vifaa vya kidijitali na nyenzo za hatia" (vitabu na vifaa vya kuandikia tunavyodhania). Kabla ya uvamizi huu, Jharkhand (jimbo) ATS ilikuwa imewaweka kizuizini watu wawili kuhusiana na kesi ya Hizb ut Tahrir. Serikali ya India ilipiga marufuku kinyume cha sheria Hizb ut Tahrir mnamo tarehe 10 Oktoba 2024, ikitaja juhudi zake za kusimamisha "Khilafah" ya kimataifa kupitia ugaidi na itikadi kali.

Soma zaidi...

Wadhifa wa Rais eneo la Asia ya Kati ni Sawia na Ufalme

Shirika la habari la Radio Liberty liliripoti mnamo tarehe 29 Mei: "Putin alifanya mazungumzo na Rustam Emomali, mwenyekiti wa bunge kuu la Tajikistan. Katika mfumo wa ziara yake rasmi jijini Moscow, Mwenyekiti wa Majlisi Milli Majlisi Oli ya Tajikistan na Meya wa Dushanbe Rustam Emomali walifanya mazungumzo na Rais wa Urusi Vladimir Putin, Spika wa Baraza la Federali Valentina Matvienko na Mwenyekiti wa Jimbo la Duma Vyacheslav Volodin.

Soma zaidi...

Ziara ya Usaliti

Katika wakati ambapo ulimwengu wa Kiislamu unavuja damu—kuanzia Gaza hadi Kashmir, hadi barabara za Tehran—ziara ya Jenerali Asim Munir kwa Rais wa Marekani Donald Trump si tu kwamba ni uziwi bali ni usaliti wa kiasi kikubwa. Mkutano huo, uliofanyika katika Ikulu ya White House na uliandaliwa na Trump kama ishara ya kushukuru dori ya Munir katika kutuliza hali iliyokaribia vita na India, inasifiwa na sehemu za utawala wa Pakistan kama hatua ya kimkakati ya kidiplomasia.

Soma zaidi...

Tanzia ya Mbebaji Ulinganizi: Ustadh Hassan Nouair

Hizb ut Tahrir katika Wilaya ya Tunisia inaomboleza kifo cha mmoja wa watu wake miongoni mwa Wabebaji Da’wah, Ustadh Hassan Nouair, aliyefariki dunia leo, Ijumaa, tarehe 24 Dhu al-Hijjah 1446 H, sawia na 20/06/2025 M, baada ya mapambano na maradhi ambayo yalidhoofisha mwili wake lakini hayakuzima moto wa ujumbe wake wala azma yake ya kufanya kazi katika safu za wale wanaojitahidi kuregesha mfumo kamili wa maisha wa Kiislamu kwa kusimamisha Khilfah Rashida kwa njia ya Utume.

Soma zaidi...

Tanzia ya Mbebaji Ulinganizi: Mabrouk Ben Nasser

Hizb ut Tahrir / Wilayah Tunisia inaomboleza kwa huzuni na majonzi makubwa kuondokewa na ndugu yetu Mabrouk Ben Nasser, aliyefariki siku ya Alhamisi, 23 Dhu al-Hijjah, 1446 H, sawia na 19 Juni 2025 M. Alikuwa mmoja wa Mashababu (wanachama) wa Hizb ut Tahrir ambao walifanya kazi ndani ya safu zake wakati wa nyakati za giza za dhulma na ukandamizaji, akiwa amezuiliwa kwenye jela za Bourguiba na kisha Ben Ali. Alitumia muda wake kwa subira na imani, akiendelea kushikamana na ulinganizi wake na kujitolea kuubeba, akilingania Khilafah Rashida kwa njia ya Utume.

Soma zaidi...

Ni kutokana na Usaliti wa Watawala Vibaraka wa Ulimwengu wa Kiislamu ambapo Wakatili Wawili wa Amerika - Umbile la Kiyahudi katika Ardhi za Kiarabu na India ya Hindutva huko Asia Kusini - wanaonyesha Kusubutu kwao Kukiuka Ubwana wa Ardhi za Kiislamu

Hizb ut Tahrir / Wilayah Bangladesh, leo (Juni 20, 2025) Ijumaa baada ya swala ya Ijumaa, iliandaa maandamano katika misikiti mbalimbali ya Dhaka na Chittagong kupinga kuendelea kwa mauaji ya halaiki huko Gaza ikiwa ni pamoja na kuzuiliwa kwa chakula na shambulizi dhidi ya Iran na umbile nyakuzi la kiyahudi.

Soma zaidi...

“Baada ya Kuibuka kwa (Israel) Tulikabiliana na Ulimwengu wa Kiarabu Ulioungana, na Polepole Tukaugawanya”

Kwa maneno haya, Netanyahu anahutubia watu wake na ulimwengu, akijigamba kana kwamba amefanya hivyo. Kama ilivyo desturi ya watu wake, ni wachongezi, waongo na kudai wasichokuwa nacho! Kabla ya kuwepo kwa umbile la wale ambao Mwenyezi Mungu amewalaani na kabla ya kuvunjwa kwa Khilafah, “Ulimwengu wa Kiarabu” haukuunganishwa tu. Badala yake, ulikuwa ni umma mmoja chini ya dola moja. Umma huu haukugawanywa na nyinyi, bali mabwana zenu waliokubuni kwa uovu na hila. Mabwana wenu waliopigana na umma huu kwa karne nyingi, wakionja nguvu zake na kushuhudia kuanguka kwa miji yao mikuu mmoja baada ya mwingine. Konstantinopoli ilitekwa na dada yake (Roma) karibu kuanguka, lakini Mwenyezi Mungu akataka ibaki kuwa hifadhi kwa ushindi mpya ujao, Inshallah.

Soma zaidi...

Umbile la Kiyahudi ni Panya Anayejifanya Kumiliki Nguvu ya Simba, Ubabe na Ujasiri wake unatokana na Watawala Wasaliti wa Waislamu

Alfajiri ya Ijumaa, 13/6/2025, umbile la Kiyahudi lilifanya mashambulizi ya kushtukiza dhidi ya Iran, yakilenga maeneo ya nyuklia na makao makuu ya kijeshi, na kusababisha vifo vya viongozi kadhaa wa kijeshi na usalama, pamoja na wanasayansi wa nyuklia.

Soma zaidi...

Majibu ya Aibu ya Tawala katika Nchi za Waislamu kwa Uvamizi wa Umbile la Kiyahudi dhidi ya Iran!

Yeyote anayetazama miitikio ya tawala zilizopo katika ardhi za Waislamu kwa mashambulizi ya umbile la Kiyahudi dhidi ya Iran atahisi huzuni kubwa na masikitiko kwa hali ya sasa ya Waislamu. Wengine wamelaani na kushutumu pekee; wengine wameonyesha hofu ya machafuko katika eneo hilo kutokana na mashambulizi haya. Baadhi walieleza kuwa ni ongezeko la hatari; wengine walielezea wasiwasi wao juu ya athari zake kwa kadhia ya Palestina. Wengine hata walitangaza kuwa tayari kufanya upatanishi kati ya Iran na umbile la Kiyahudi. Walio bora zaidi walionyesha nia ya kuiunga mkono Iran katika majukwaa ya kimataifa, huku baadhi ya nchi hizo hizo zikifungua anga zao kwa ndege za umbile la Kiyahudi kuruka juu, kuipiga Iran kwa mabomu, kuua na kuharibu, na kisha kuregea bila hata risasi moja kufyatuliwa kwao! Wengine walinasa makombora na droni za Iran zilizolenga kushambulia umbile la Kiyahudi, na hivyo kuwaepusha na kupigwa!

Soma zaidi...

Enyi Waislamu: Adui Yenu Anaujua Uzito Wenu Vizuri Kuliko Mnavyoujua nyinyi, na Anakuogopeni Nyinyi na Anakuchukulieni Kwa Umakini Mara Elfu!

Siku baada ya siku, matukio na misimamo inafichua ushahidi mwingi wa dola za kikoloni za kikafiri kuwaogopa Waislamu, ikiwemo umbile vamizi la Kiyahudi. Pia inaonyesha kwamba wanapoamiliana na Waislamu, wanawachukulia kwa uzito mara elfu moja. Baada ya zaidi ya karne moja, baada ya kuvunjwa kwa Khilafah, kugawanyika kwa Waislamu na kuwa maumbo dhaifu, nyenyekevu, ikifuatwa na udanganyifu na uvamizi wa kifikra, kujitenga kwa Waislamu na imani yao, kuporwa mali ya Waislamu, kupanuka kwa ushawishi wa wakoloni hao makafiri katika ardhi zao, na kudhoofika kwao na kudhalilika, baadhi wanasema: Waislamu kamwe hawatainuka tena, na baada ya haya yote, tunasikia na kuona kauli kutoka kwa viongozi wa Magharibi na viongozi wa umbile vamizi la Kiyahudi, ambazo zinaonyesha hofu yao ya Uislamu na hofu iliyojaa nyoyoni mwao kutoka kwa Waislamu katika hali hii.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu