Jumamosi, 05 Muharram 1448 | 2026/06/20
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Vyombo vya Usalama katika Mji wa Al-Qadarif Vyawakamata Mashababu wa Hizb ut Tahrir vikiliunga mkono umbile la Kiyahudi!

Katika hotuba ya hadhara iliyotolewa na Mashababu wa Hizb ut Tahrir katika mji wa Al-Qadarif, kwenye soko la Al-Qadarif karibu na hospitali ya meno, mnamo siku ya Alhamisi, tarehe 23 Dhul-Hijjah 1446 H, inayolingana na 19/6/2025 M, Ustadh Awad Muhajir, mwanachama wa Hizb ut Tahrir, alizungumza kuhusu uhalisia wa vita na umbile la Kiyahudi, furaha ya Waislamu kwa mashambulizi dhidi ya umbile hili, na kiu ya watu ya ushindi dhidi ya mkaaji huyu wa kimabavu wa ardhi tukufu—Masrah ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw). Alithibitisha faradhi ya kusimamisha Khilafah Rashida kwa njia ya Utume, ambayo itaikomboa Palestina na ardhi nyenginezo za Kiislamu zinazokaliwa kwa mabavu. Hadhira iliitikia vyema hotuba hiyo, na kulikuwa na michangio tofauti tofauti kutoka kwa waliohudhuria.

Soma zaidi...

Mkataba wa Yunus-Tarique wa London ni Jaribio la Kudumisha Utawala wa Marekani na Mfumo wao Kandamizi wa Kisekula wa Kibepari

Mnmo tarehe 13 Juni 2025, mkuu wa serikali ya mpito Dkt. Yunus, akiwa amkeketi jijini London, amewakatisha tamaa wananchi kwa kufanya maridhiano ya kisiasa na Tarique Rahman, kaimu mwenyekiti wa BNP (Bangladesh Nationalist Party) kwa sababu watu wa nchi hii hawajasahau historia ya utawala mbaya na ufisadi wa matabaka tawala ya BNP. Kwa hakika, maridhiano haya ya kisiasa ya Yunus-Tarique na kugawanya madaraka ni sehemu ya mpango wa Marekani, ambao kupitia kwao wataweza kutekeleza miradi ya kikoloni. Mumeshuhudia kwamba waliokuwa mabalozi wa Marekani Dan Mozena, Bernicat na Peter Hass, wote wamekaribisha maridhiano haya na kuonesha kuridhika, na kwa mujibu wa taarifa za habari, BNP pia imependekeza kumfanya Dkt. Yunus kuwa rais. Kupitia kuanguka kwa dhalimu Hasina, watu wa nchi hii walionyesha nia yao ya kutaka kuwa huru kutokana na mfumo dhalimu wa kibepari na kutawaliwa na Wakoloni makafiri wa Magharibi. Aina hii ya maridhiano si lolote bali ni usaliti kwa watu wa nchi hii.

Soma zaidi...

Na Mwenyezi Mungu si mwenye Kughafilika na Wanayoyafanya Madhalimu

Tunaona kwamba vyombo vya usalama vya dola nchini Kyrgyzstan vinawakamata wahalifu ambao wamefanya uhalifu mbalimbali, na baadhi yao walishtakiwa kuwa katika genge la wahalifu, huku wengine wakishtakiwa kwa hongo, mauaji, na mashtaka mfano wa hayo. Ikiwa kweli wanahusika katika uhalifu huo, basi wanachukuliwa pia kuwa wahalifu kwa mujibu wa Shariah ya Kiislamu. Lakini wakati huo huo, tunashuhudia kwamba kuna wafungwa ambao hawakufanya kitendo chochote cha jinai, bali walikamatwa kwa sababu tu ya kulingania dini ya Mwenyezi Mungu na kwa kusema: “Mola wetu ni Mwenyezi Mungu”! Na pia wanakamatwa kikatili mithili ya wahalifu wa kweli na kutupwa magerezani ambako hupigwa sana na mbinu nyingine za "kisasa" za mateso. Hawa ni wanachama wa Hizb ut Tahrir, na madhalimu ni maafisa wa serikali na vyombo vyao vya usalama.

Soma zaidi...

Jinsi Viongozi wa Waislamu Wanavyoitelekeza Gaza kwa ajili ya Diplomasia na Miamala

Rais wa Indonesia Prabowo Subianto alihimiza kusitishwa kwa mapigano mara moja kati ya 'Israel' na Hamas, na akatoa wito wa kusitishwa kwa mzozo wa 'Israel' na Iran. Akizungumza nchini Singapore na Waziri Mkuu Lawrence Wong, Prabowo alisisitiza haja ya azimio la amani kupitia diplomasia. Alionyesha wasiwasi wake mkubwa juu ya vifo vya raia huko Gaza na kuongezeka kwa mvutano katika Mashariki ya Kati. Zaidi ya hayo, alizungumzia mzozo wa Myanmar, akisisitiza kujitolea kwa ASEAN kwa Makubaliano ya Mambo Tano ya kukomesha vurugu na kukuza mazungumzo jumuishi. Indonesia na Singapore zilikubali kuendelea kuunga mkono ushirikiano wa amani nchini Myanmar na kuzingatia kanuni za ASEAN za uthabiti wa kikanda na juhudi za kibinadamu.

Soma zaidi...

Kuharibu Masoko kama vile Soko la Dokhinat ni Vita dhidi ya Watu katika Riziki zao na ni Matokeo ya Kukosekana kwa Dola ya Kiislamu ya Khalifah

Katika kitendo cha kikatili na vurugu, mamlaka za eneo la Jabal Awlia, Jimbo la Khartoum, kwa kutumia askari waliokuwa na silaha nyingi, walibomoa Soko la Tumbaku lililoko kwenye Barabara ya Jabal Awlia kwa tingatinga mnamo siku ya Alhamisi asubuhi, 12 Juni 2025, na kuvunja meza za maonyesho. Hata wale waliotoroka soko hilo na bidhaa zao hawakusazwa!

Soma zaidi...

Kati ya Usaliti wa Palestina na Kashmir na Utumwa kwa Amerika Asim Munir Anafanya Nini Mbele ya Firauni Wa Zama Zetu, Trump?

Katika wakati ambapo Amerika inapigana vita dhidi ya jirani Muislamu, Iran, kwa kutumia mkono wake mchafu katika eneo hilo, umbile la Kiyahudi, Rais wa Marekani, Donald Trump, alimkaribisha Mkuu wa Majeshi wa Pakistan mnamo Jumatano, 18 Juni 2025, kwa chakula cha mchana katika mkutano ambao haujawahi kushuhudiwa katika Ikulu ya White House. Kinachotia shaka kuhusu mkutano huu, na muda wake, ni kwamba ni mara ya kwanza kwa rais wa Marekani kumkaribisha mkuu wa jeshi la Pakistan katika Ikulu ya White House, bila ya kuwepo kwa afisa yeyote mkuu wa kiraia wa Pakistan, kuashiria umuhimu wa mkutano huo, na unyeti wa mada yake.

Soma zaidi...

Kauli zilizotolewa na Waziri Mkuu Nawaf Salam kuhusu Hamu yake ya Kuhalalishwa Haraka kwa Mahusiano na Mayahudi Haziwawakilishi Waislamu kwa vyovyote vile! Badala yake, zinamwakilisha yeye na wale waliomleta madarakani. Kauli hizi ni khiyana kwa Mwen

Katikati ya angahewa Amerika inaenea katika eneo hili kupitia kwa rais wake Trump, akitoa wito wa amani na Mayahudi, na kwa mujibu wa Makubaliano ya Abraham yaliyokuja wakati wa ziara yake ya kuchukiza katika eneo hilo, na kujisalimisha kwa watawala wa Kiarabu na Waislamu kwenda sambamba na ajenda hii, hadi kufikia kiwango ambacho mbora zaidi kati yao anaweza kusema ni "tutakuwa wa mwisho kuhalalisha mahusiano na Mayahudi", katika muktadha huu wa Mahojiano Waziri Mkuu wa Lebanon Nawaf Salam wakati wa mahojiano na Mtandao wa CNN, yaliyochapishwa mnamo 30/5/2025, ambapo alisema: "Uhalalishaji mahusiano ni sehemu muhimu ya amani tunayotaka kuona kesho, sio kesho kutwa!"

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu