Uhakiki wa Habari 23/08/2023
- Imepeperushwa katika Vichwa vya Habari
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Viongozi na maafisa wakuu kutoka mataifa matano yenye uchumi unaoinukia duniani walikutana jijini Johannesburg kwa mkutano wa siku tatu wa BRICS. Jumuiya hiyo—ambayo wanachama wake ni Brazil, Urusi, India, China, na Afrika Kusini—inawakilisha asilimia 40 ya watu wote duniani na robo ya Pato lake la Taifa.



