Jarida la Al-Waie: Vichwa Vikuu vya Habari vya Toleo 436
- Imepeperushwa katika Jarida la Al-Waie
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
Katika hatua ya kuwapa mikopo wafanya biashara wadogo wadogo ambao wamekuwa wakitaabika kuchukua mikopo katika benki kubwa, serikali imezindua mfuko wa fedha unaojulikana maarufu Hustler Fund ambapo baada tu ya uzinduzi huo takriban Wakenya milioni 17 tayari wamechukua mkopo huo kwa muda tu wa saa moja kwenye siku ya kwanza ya uzinduzi huo.
Mwishoni mwa karne ya kumi na nane na kumi na tisa sayansi ilikuzwa kama ufunguo wa maendeleo na baadaye ilinasibishwa na hadhara. Auguste Comte katika kazi yake aliripoti katika ‘The Course of Positive Philosophy’ jamii ililengwa kurekebishwa kwa msingi wa kisayansi.
Je, munamjua muulizaji ni nani? Wakasema Mwenyezi Mungu na Mtume wake wanajua zaidi. Akasema: Huyu ni Jibril amekuja kukufunzeni Dini yenu. Hii ni khabar ahaad katika Aqida, basi ni kwa nini tunaikataa?
Chama cha Republican kilipata udhibiti, kwa wingi mdogo, juu ya Baraza la Wawakilishi la Marekani ambalo lina viti 435. [“Kilishinda angalau viti 218, kulingana na makadirio ya CBS News, mshirika wa BBC nchini Marekani.” (BBC, Novemba 17, 2022)]. Kuhusu Wanademokrasia, walisherehekea [“Jumapili kwamba chama kilibakisha wingi wa watu wengi katika Seneti ya Marekani,”
Kuna mkanganyiko miongoni Wakenya wengi ya kuwa je ilikuwa ni busara kwa uamuzi wa serikali wa kuondosha marufuku ya vyakula vinavyotokana na mazao ya kisaki (GMO). Katika taifa ambalo kila mwaka hukumbwa na uhaba wa chakula unaosababishwa na mambo kadhaa ikiwemo ukame uliosababisha mamilioni ya Wakenya kukabiliwa na baa la njaa kila mwaka, dhana iliyoko ni kwamba vyakula vya GMO ni hatari kwa afya ya mwanadamu na katika kuendesha vyema kilimo.
Serikali ya Urusi ilijibu hadharani kuimarisha uhusiano kati ya serikali ya Uzbekistan na Marekani. Hii ilikuwa wakati wa ziara ya Spika wa Jimbo la Duma la Urusi, Vyacheslav Volodin, huko Uzbekistan, ambayo ilianza Novemba 27, na katika tangazo rasmi la mwisho wa ziara hiyo lililowekwa kwenye tovuti ya Jimbo la Duma la Shirikisho la Urusi.
Bi kizee mmoja wa Marekani mwenye umri wa miaka 87 alikamatwa hadharani kwa kutolipa bili ya ukusanyaji wa taka. Faini ya dolari 77 iliyokuwa haijalipwa ilizingatiwa inastahili zaidi kwa maafisa wawili kumkamata nyumbani kwake asubuhi, kumtia pingu hadharani na kumpeleka gerezani. Aliwekwa katika seli ndogo kwa siku nzima hadi kuachiliwa kwake kulipojadiliwa.
“Mwanadiplomasia wa Kiyahudi alionyesha wasiwasi wake juu ya kukosekana uhalalishaji mahusiano na makubaliano ya amani, yaliyotiwa saini na umbile la Kiyahudi pamoja na baadhi ya watawala wa nchi za Kiarabu, na watu wa nchi hizo. Ilionekana wazi katika Kombe la Dunia nchini Qatar kwamba watu wanakataa uhalalisha mahusiano na mvamizi huyo.”
Indonesia imepitisha kanuni mpya ya jinai yenye ubishani inayojumuisha kupiga marufuku kuishi kinyumba na ngono nje ya ndoa, katika mabadiliko ambayo wakosoaji wanashindana yanaweza kuhujumu uhuru katika taifa hilo la Asia ya Kusini. Sheria hizo mpya zinahusu watu wa Indonesia na wageni na pia zinaregesha marufuku ya kumtusi rais, taasisi za serikali au mfumo wa kitaifa wa Indonesia unaojulikana kama Pancasila.