Ijumaa, 29 Jumada al-thani 1447 | 2025/12/19
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Iwapo Kuanguka kwa ‘Jamhuri’ Hakukupelekea Kusimamishwa kwa Khilafah, Ni lazima Kutumike kama Hatua ya Mpito kuelekea Khilafah Rashida

Kuporomoka kwa serikali ya Jamhuri nchini Afghanistan ni moja ya matukio muhimu zaidi kwa watu wa Afghanistan na Umma mpana wa Kiislamu katika karne ya 21. Serikali hii sio tu kwamba haikuwa na mizizi yoyote katika itikadi ya Kiislamu, bali ilikuwa ni zao la muundo wa ukoloni mamboleo - mfumo ulioagizwa kutoka nje uliojengwa ili kurasimisha ufisadi, utegemezi, na dhulma. Kuanguka kwake lilikuwa ni mwisho wa kimaumbile na usioepukika wa mfumo ambao, tangu kuanzishwa kwake, ulikuwa ngeni kwa kitambulisho cha Kiislamu na kupingana na maadili ya Uislamu.

Soma zaidi...

Ayman Safadi: “Yeyote ambaye ana badali ya Suluhisho la dola mbili, basi na aiwasilishe!” Hizb ut Tahrir imewasilisha na inaendelea kuwasilisha suluhisho halali na la kivitendo

Serikali ya Jordan ndio iliyowawekea watu wa Jordan na Umma wa Kiislamu suluhisho linaloendana na kuhifadhi usalama wa umbile katili la Kiyahudi. Hukuwa na maregeleo ya masuluhisho ya kadhia ya Palestina isipokuwa Marekani, rafiki wa serikali hii, mshirika wa umbile la Kiyahudi, mdhamini wake, mlinzi wake, na mshirika wake katika vita vya maangamizi na njaa dhidi ya watu wa Gaza.

Soma zaidi...

Kauli za Netanyahu kuhusu "Israel Kubwa" ni Tangazo la Vita ambalo linafuta Mikataba, na, kwa sababu hiyo, Majeshi Yanasonge, na Jambo jengine lolote lisokuwa hilo ni Usaliti

Huyu hapa mhalifu wa kivita Netanyahu anatangaza waziwazi na bila kufasiriwa kwa watawala waoga wa Kiarabu na wasemaji wao, akisema katika mahojiano na chaneli ya Kiebrania i24: “Mimi niko kwenye misheni ya vizazi na kwa jukumu la kihistoria na la kiroho, ninaamini kwa dhati ruwaza ya Israel Kubwa, ambayo ni pamoja na Palestina ya kihistoria na sehemu za Jordan na Misri.” Mhalifu Smotrich alikuwa amemtangulia kwa kauli zile zile na kunyakua sehemu za nchi za Kiarabu zinazoizunguka Palestina, ikiwemo Jordan. Katika muktadha huo huo, adui namba moja wa Uislamu na Waislamu, Rais Trump wa Marekani, alimpa idhini ya upanuzi wake akisema, “Israel ni sehemu ndogo sana ikilinganishwa na ukubwa wa ardhi hizo, na najiuliza ikiwa inaweza kupata ardhi zaidi kwa sababu kweli ni ndogo sana.”

Soma zaidi...

Kuundwa kwa cheo cha "Mufti Muongofu" katika Zama za Akili Bandia Kuunda Sheria Inayoafikiana na Magharibi na Watawala wake Vibaraka

Katikati ya mporomoko wa kisiasa na kifikra wa Umma wa Kiislamu, na wakati ambapo njama dhidi ya dini yake na hukmu zake zikiongezeka, serikali tawala na zana zao - taasisi rasmi za kidini - zinazindua makongamano yenye kauli mbiu za kustaajabisha na misamiati ya uchochezi ya kiteknolojia, wakikopesha mradi wao wa kupotosha kuwa dini ni kero kwa “usasa” na “maendeleo”. Hii ni pamoja na kongamano la "Kuunda cheo cha Mufti Sahihi Katika Zama za Akili Bandia,” lililoandaliwa na Dar al-Ifta ya Misri chini ya udhamini wa moja kwa moja wa Rais Abdel Fattah el-Sisi.

Soma zaidi...

Msako Mkali wa Amerika dhidi ya Mashirika ya Kiislamu

Katika mahojiano ya hivi majuzi na mtangazaji wa redio Sid Rosenberg, Katibu wa Waziri wa Mambo ya Nje Marco Rubio alionyesha mchakato unaoendelea wa kuiorodhesha Ikhwan al-Muslimin na CAIR kama mashirika ya kigaidi. Waziri Rubio alisema kwamba uorodheshaji kama huo ulikuwa "katika kazi zao, na ni wazi kuna matawi tofauti tofauti ya Ikhwan al-Muslimin, kwa hivyo itabidi uliorodheshe kila moja yao."

Soma zaidi...

Gaza iko Ukingoni mwa Kuzidishwa Mauaji na Ukandamizaji Mkali ikiwa Umma wa Kiislamu hautasonga mbele Kuinusuru

Gaza Hashim inaingia katika hatua mpya ya mauaji na uharibifu baada ya wizara ya usalama ya umbile halifu kuamua asubuhi ya Ijumaa hii, 08/08/2025, kupanua operesheni zake ili kuweka udhibiti wake juu ya Mji wa Gaza kikamilifu, na uamuzi huu ulikuja kwa siri kutoka kwa Amerika kwa ulimi wa Trump, Rubio, na wengine kutoka kwa wakaazi wa (ikulu ya) Jumba Jeusi.

Soma zaidi...

Kukipokonya Silaha Chama cha Iran na Dori ya Mamlaka ya Lebanon!

Makubaliano ya kusitisha mapigano ya tarehe 27/11/2024, kati ya umbile la Kiyahudi na mamlaka za Lebanon, chini ya usimamizi wa moja kwa moja wa Marekani, yaliweka msingi wa kisiasa wa kukipokonya silaha chama cha Iran na mirengo mengine ya Palestina nchini Lebanon. Hii haikuwa kutokana na kutaka "amani" kutoka Marekani, bali ni kuhakikisha usalama wa umbile la Kiyahudi katika maandalizi ya kuondoa uwezo mdogo uliobaki wa Waislamu wa kupigana nao, hasa baada ya matukio ya Kimbunga cha Al-Aqsa.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu