Ijumaa, 17 Ramadan 1447 | 2026/03/06
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Hizb ut Tahrir/ Wilayah Pakistan: Gaza inahitaji kuingia kwa majeshi ya Waislamu, sio tu misaada ya kibinadamu!

Taarifa ya mwisho ya Mkutano wa Waarabu, ulioandaliwa na mji mkuu wa Iraq, Baghdad mnamo tarehe 17 Mei 2025, ilisisitiza haja ya kuleta misaada ya kibinadamu mjini Gaza. Watawala wa Waislamu, Waarabu na wasiokuwa Waarabu, wamezuia majeshi ya Waislamu kupigana na Mayahudi, kwa zaidi ya mwaka mmoja na nusu. Mtume ﷺ ametuambia kuwa kupigana na Mayahudi na kuwashinda kunaleta malipo makubwa.

Soma zaidi...

Kudumu kwa Mashirika ya Kifeministi na Mashoga hadi kufikia Hatua ya Kueneza Uchafu miongoni mwa Waumini ni Shambulizi la Dhahiri kwa Heshima ya Waislamu

Baada ya wasagaji wawili wanachama wa chama chenye uhusiano na Chuo Kikuu cha Marekani cha Beirut (AUBMC), chini ya kivuli na jina "Programu Oanishi ya Afya ya Jimai ya Wanawake (WISH) katika AUBMC," kutembelea shule ya upili ya wasichana jijini Tripoli, kwa uratibu wa Wizara ya Elimu; kisha kwa mbwembwe na bila aibu kuendekeza mambo machafu na kuonyesha picha na maudhui machafu kwa wanafunzi, wazazi wakasukumwa kuripoti tukio hilo kwa uongozi wa shule, ambao nao ulieleza kuwa wawili hao walikuja shuleni kwa amri ya Wizara ya Elimu na Elimu ya Juu!

Soma zaidi...

Serikali Yalazimisha Watu Kusherehekea Uhuru Unaodaiwa Sambamba na Mauaji ya Kikatili ya Halaiki!

Je, watu wa Jordan wanasherehekea uhuru unaodaiwa wakati jana, daktari Muislamu mwenye msimamo thabiti huko Gaza alipoteza watoto wake tisa wote kwa wakati mmoja, kutokana na kombora lililorushwa na ndege ya jeshi la mauaji ya halaiki nyumbani kwao, katika mandhari ya kinyama isiyo na kifani katika historia ya mwanadamu?

Soma zaidi...

Wananchi Wanataka Kupinduliwa kwa Serikali na Kusimamishwa kwa Utawala wa Kiislamu

Aden, mji mkuu wa muda wa serikali ya Yemen, umeshuhudia maandamano matatu ya wanawake na wanaume katika wiki mbili zilizopita. Kutokana na mateso yanayoendelea kwa wananchi, maandamano ya hasira yamefanyika mjini Aden, wakidai huduma za msingi na kukemea hali ngumu ya maisha na huduma duni. Maandamano haya yalijumuisha kauli mbiu dhidi ya muungano wa Waarabu, serikali ya Yemeni, na Baraza la Mpito, ambalo linadhibiti mji mkuu wa muda, Aden. Maandamano haya pia yalishuhudia milio ya risasi na kukamatwa kwa baadhi ya waandamanaji. Maandamano haya yalifanywa na wanawake na wanaume kwa siku tofauti. Kilichotia fora ni kuregea kauli mbiu isemayo “Wananchi wanataka kupinduliwa kwa serikali,” ambayo inatukumbusha Mapinduzi ya Kiarabu dhidi ya ukandamizaji na udhalimu.

Soma zaidi...

Serikali ya Muda Inatengwa na Wananchi kwa sababu ya Utiifu wao kwa Amerika; kwa upande mwingine, Msimamo wa Jeshi letu katika Kupendelea Ubwana wa Nchi kwenye Masuala ya 'Mkondo' na 'Bandari' ni Dhihirisho la Matarajio ya Watu

Huku serikali ya mpito, ikiwapuuza Waislamu wa Rohingya na ubwana wa nchi hiyo, inatamani sana kupeana 'mkondo' kwa maslahi ya kisiasa ya kijiografia ya Amerika na kukabidhi shughuli za 'New Mooring Container Terminal' kwa kampuni yenye ushawishi wa Marekani "DP World", msimamo mkali wa jeshi letu kuunga mkono ubwana wa nchi umesifiwa na watu wengi.

Soma zaidi...

Maandamano ya Kulaani yaliyoandaliwa na Hizb ut Tahrir, Wilayah Bangladesh: “Palestina, Kashmir, Arakan – Khilafah pekee ndiyo Suluhisho”

Hizb ut Tahrir / Wilayah Bangladesh, leo (23/05/2025) baada ya swala ya Ijumua, iliandaa maandamano ya kulaani katika misikiti mbalimbali ya Dhaka na Chittagong dhidi ya wimbi jipya la mashambulizi ya umbile lililolaaniwa la Kiyahudi kuchukua udhibiti wa Ukanda wote wa Gaza.

Soma zaidi...

Bunge la Ulaya na Maazimio ya Ukoloni Mambo Leo

Wiki iliyopita Bunge la Jumuiya ya Ulaya (EU) lilitoa mwito kwa Tanzania kuchukua hatua kadhaa ikiwemo kutatua kesi waliyosema ina msukumo wa kisiasa ya kiongozi wa chama cha upinzani, kutoa uhuru zaidi wa kisiasa kupitia majadiliano, kufanya mabadiliko ya sheria za uchaguzi,kuheshimu haki ya vyama kushiriki katika uchaguzi huru nk.

Soma zaidi...

Nia na Malengo ya Ziara ya Afisa wa Uingereza nchini Uzbekistan

Mnamo Mei 13, 2025, Lord Cocker, Waziri wa Ulinzi wa Uingereza, alifanya ziara rasmi nchini Uzbekistan. Ziara hii ni muhimu kwani ni ziara ya kwanza rasmi nchini Uzbekistan kwa mwakilishi wa serikali mpya ya Uingereza. Wakati wa ziara yake, alikutana na uongozi wa jeshi la Uzbekistan, akiwemo Naibu Waziri wa Ulinzi Kanali Jenerali Hamdam Qarshiyev na Kamanda wa Walinzi wa Kitaifa Luteni Jenerali Rustam Juraev. Mikutano hii ilithibitisha kujitolea kwa Uingereza katika kuimarisha ushirikiano wa ulinzi wa nchi mbili na Uzbekistan. Lord Cocker pia alitoa hotuba katika Chuo cha Jeshi la Uzbekistan, mara ya kwanza kwa Waziri wa Ulinzi wa Uingereza kuzungumza katika chuo hicho.

Soma zaidi...

Ulemavu wa Marekani huku Ikijila Yenyewe ikiwa Hai Sehemu Nyingi Zaidi

Kichwa cha habari cha Fox News mnamo tarehe 22 Mei kilisema kwamba "Utawala wa Trump wasitisha mpango wa visa ya wanafunzi wa Harvard" na makala hayo yalimnukuu Waziri wa Elimu, Kristi Noem, akisema: "Utawala huu unaihisabu Harvard kwa kuendeleza vurugu, chuki dhidi ya Mayahudi, na kuratibiana na Chama cha Kikomunisti cha China kwenye chuo chake ... Ni fursa, sio haki, kwa vyuo vikuu kuchukua wanafunzi wa kigeni na kufaidika na malipo yao ya juu ya masomo ili kusaidia kulipa ruzuku zao za mabilioni ya dolari. Harvard ilikuwa na fursa nyingi za kufanya mambo kwa usahihi. Ilikataa. Wamepoteza cheti chao cha Mpango wa Wanafunzi na Ubadilishanaji wa Wageni (Student and Exchange Visitor Programme) kutokana na kushindwa kwao kuzingatia sheria. Hebu hili na liwe ni onyo kwa vyuo vikuu na taasisi zote za kielimu kote nchini."

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu